CHATANDA: CHAMA CHA MAPINDUZI KIMEANDIKA HISTORIA MPYA. - OKULY BLOG

Breaking

Music

Header ADS

Friday, December 9, 2022

CHATANDA: CHAMA CHA MAPINDUZI KIMEANDIKA HISTORIA MPYA.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa WanawakeTanzania ya Chama cha Mapinduzi (UWT), Mary Chatanda na Makamu Mwenyekiti wa umoja huo, Zainab Shomari wakinyoosha mikono juu walipokuwa wanacheza muziki wakati wa mkutano wa kumpongeza Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Novemba 9, 2022.

Na Okuly Julius-Dodoma

IKIWA ni siku moja kupita tangu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, umoja wa wanawake Tanzania UWT kimempongeza Dkt Samia suluhu hassan kwani ni mwenyekiti wa kwanza Mwanamke Tangu Chama cha mapinduzi kianzishwe mwaka 1977.

Akizungumza kwenye Mkutano Maalum wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Mwenyekiti wa umoja wa Wanawake Taifa Marry Chatanda amesema baadhi ya wanachama na viongozi mbalimbali wamemtaja Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuwa ni mmoja wa wanamke shujaa wanaotambuliwa kimataifa kwa utendaji kazi wake wa vitendo.

Aidha, Marry chatanda amewasisitiza wanachana hao kuwa wamoja na kuvunja makundi waliokuwa nayo ambapo ametoa wito kwa Mikoa,wilaya,kata na Matawi kuhakikisha Ajenda ya kuongeza wanachama wapya wa makundi mbalimbali inakuwa ni Ajenda ya kudumu.

Umoja wa wanawake Tanzania UWT umesema Kwa kutambua kuwa Wanawake ndio nguzo ya familia, itatimiza wajibu wake katika malezi, makuzi, ustawi na maendeleo ya watoto na familia ikiwemo kuhakikisha wanadumisha maadili, desturi na tamadumi chanya kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

No comments:

Post a Comment